KWA MAWASILIANO ZAIDI TUMIA BARUA PEPE rockersports212@yahoo.com AU TUPIGIE KUPITIA NAMBARI 0767166607 AU 0717166607. KARIBU SANA. 66666666607 AU 0717166607

Wednesday, January 8, 2014

Football: Jerome Valcke anasema Kombe la dunia 2022 huenda likahamishiwa miezi ya Novemba nchini Qatar

Baridi: FIFA imependekeza kuwa kombe la dunia 2022 lichezwe kati ya Novemba na Januari. Picha ya juu ni mchoro wa  uwanja wa Al Gharafa ambapo unapendekezwa na wenyeji kutumika katika fainali hizo

Katibu mkuu wa shirikisho la soka duniani FIFA amesema kuwa michuano ya kombe la dunia 2022 nchini Qatar halitafanyika tena mwezi June au July.
Jerome Valcke, ambaye alipewa kazi ya kutafuta tarehe mbadala ya kufanyika kwa fainali hizo kutokana na kuaminika kuwa katika cha miezi hiyo hali ya juu joto huwa ni kali kupindukia nchini Qatar, amesema kuna uwezekanao wa fainali hizo zikachezwa kati Novemba 15 na Januari 15.
Valcke ameiambia redio France Info ya nchini Ufaransa kuwa 'haitakuwa tena mwezi June au July. Ki ukweli nadhani itakuwa ni kati ya Novemba 15 na Januari 15 angalau.
'kama utachezwa kati ya Novemba 15 na mwisho wa mwaka ambapo hali ya hewa inakuwa yakuridhisha'
Valcke amependekeza  hiyo kwa kuongeza kuwa hali hiyo ni kama kipindi cha majira ya joto barani Ulaya ambapo kunakuwa na nyuzi joto 25 hivyo inafaa kwa kuchezwa mpira wa miguu'.

Hata hivyo maoni hayo ya Valcke yatahitaji kuridhiwa na kamati  ya utendaji ya FIFA.
Hata hivyo FIFA imesema katika taarifa yake kuwa hayo ni maoni binafsi ya Valcke na isichukuliwe hiyo kama ndio maamuzi yake.

Taarifa hiyo ya FIFA imeendelea kusema kuwa hakuna maamuzi yatakayo fikiwa kabla ya michuano ya kombe la dunia lijalo nchini Brazil ambapo kamati yake ya utendaji itaketi

No comments:

Post a Comment