KWA MAWASILIANO ZAIDI TUMIA BARUA PEPE rockersports212@yahoo.com AU TUPIGIE KUPITIA NAMBARI 0767166607 AU 0717166607. KARIBU SANA. 66666666607 AU 0717166607

Saturday, January 25, 2014

Wazee wa Uturuki waendelea kushikilia usukani wa msimamo wa ligi baada ya ushindi dhidi ya Ashant

Young Africans imeanza vizuri mzuguko wa pili wa Ligi Kuu ya Vodacom Tanzania bara baada ya kuibuka na ushindi wa mabo 2-1 dhidi ya timu ya Ashanti United katika mchezo wa fungua dimba uliofanyika katika dimba la Uwanja wa Taifa jijini Dar es salaam.
Timu zote zilicheza kwa kushambuliana kwa zamu lakini mpaka dakika 45 za kipindi cha kwanza zinamalizik hakuna timu iliyoweza kuliona lango wa timu nyingine kutokana na washambuliaji wa timu zote mbili kutokua makini katika umaliziaji.
Dakika ya 51 Young Africans ilipata bao la kwanza kupitia kwa mshambuliaji wake Didier Kavumbagu ambaye alimalizia kazi nzuri iliyokuwa na kiungo Saimon Msuva aliyewatoka walinzi wa Ashanti pamoja na mlinda mlango Daud Mwasongwe na kupasia Kavumbagu ambaye aliukwamisha mpira wavuni.
Dakika 61 ya mchezo Ashanti United walipata bao la kusawzisha kupitia kwa mshambuliaji Bright Obinna aliyemalizia krosi ya mshambuliaji Hussein Sued aliyemtoka mlinzi wa kulia wa Young Africans na kupiga krosi hiyo iliyomkuta mfungaji Obinna.
David Luhende aliipatia Young Africans bao la pili la mchezo dakika ya 80 baada ya kuwatoka walinzi wa Ashanti mpaka ndani ya eneo la hatari na kuachia shuti kali ambalo lilimshinda mlinda mlango wa Ashanti United na kujaa wavuni.
Mpaka dakika 90 za mchezo zinamalizika, Young Africans 2 - 1 Ashanti United.
Mara baada ya mchezo huo kocha mkuu wa Young Africans mholanzi Hans Van Der Pluijm alisema kikubwa anashukuru timu yake imepata pointi tatu, lakini kimchezo haikucheza vizuri hiyo inatokana na uchovu wa safari na mabadiliko ya hali ya hewa na kusema mchezo unaofuata vijana wake watakuwa vizuri tayari.
"Ukitazama jinsi walivyokuwa wakicheza katika mechi za nchini Uturuki na walivyocheza ni tofauti, siwezi kuwalaumu lakini kikubwa natambua wamechoka, wana uchovu wa safari kwani wamepumzika masaa 15 tu kabla ya mchezo na hali ya hewa waliyotoka ni baridi na hapa ni joto hivyo naamini baada ya siku chache watakuwa wamerejea katika hali zao za kawaida" alisema Hans.

No comments:

Post a Comment